Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 15:28-31 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Basi, Roho Mtakatifu na sisi tumekubali tusiwatwike mzigo zaidi ya mambo haya muhimu:

29. Msile vyakula vilivyotambikiwa vinyago; msinywe damu; msile nyama ya mnyama aliyenyongwa; na mjiepushe na uasherati. Mtakuwa mmefanya vema kama mkiepa kufanya mambo hayo. Wasalaam!”

30. Baada ya kuwaaga, hao wajumbe walielekea Antiokia ambako waliita mkutano wa waumini, wakawapa hiyo barua.

31. Walipoisoma hiyo barua, maneno yake yaliwatia moyo, wakafurahi sana.

Kusoma sura kamili Matendo 15