17. Hapo watu wengine wote,watu wa mataifa yote niliowaita wawe wangu,watamtafuta Bwana.
18. Ndivyo asemavyo Bwana,aliyefanya jambo hili lijulikane tangu kale.’
19. “Kwa hiyo, uamuzi wangu ni huu: Tusiwataabishe watu wa mataifa wanaomgeukia Mungu.
20. Bali tuwapelekee barua kuwaambia wasile vyakula vilivyotiwa unajisi kwa kutambikiwa vinyago vya miungu; wajiepushe na uasherati; wasile mnyama yeyote aliyenyongwa, na wasinywe damu.
21. Kwa maana kwa muda mrefu maneno ya Mose yamekuwa yakihubiriwa katika kila mji na kusomwa katika masunagogi yote kila siku ya Sabato.”