Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 15:13-21 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Walipomaliza kuongea, Yakobo alianza kusema: “Ndugu zangu, nisikilizeni!

14. Simoni ameeleza jinsi Mungu hapo awali alivyojishughulisha na watu wa mataifa mengine, akachagua baadhi yao wawe watu wake.

15. Jambo hili ni sawa kabisa na maneno ya manabii, kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:

16. ‘Baada ya mambo haya nitarudi,na kujenga tena kile kibanda cha Daudi kilichoanguka;nitayatengeneza magofu yake na kukijenga tena.

17. Hapo watu wengine wote,watu wa mataifa yote niliowaita wawe wangu,watamtafuta Bwana.

18. Ndivyo asemavyo Bwana,aliyefanya jambo hili lijulikane tangu kale.’

19. “Kwa hiyo, uamuzi wangu ni huu: Tusiwataabishe watu wa mataifa wanaomgeukia Mungu.

20. Bali tuwapelekee barua kuwaambia wasile vyakula vilivyotiwa unajisi kwa kutambikiwa vinyago vya miungu; wajiepushe na uasherati; wasile mnyama yeyote aliyenyongwa, na wasinywe damu.

21. Kwa maana kwa muda mrefu maneno ya Mose yamekuwa yakihubiriwa katika kila mji na kusomwa katika masunagogi yote kila siku ya Sabato.”

Kusoma sura kamili Matendo 15