Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 15:12-16 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Kikundi chote kilikaa kimya, kikawasikiliza Barnaba na Paulo wakieleza miujiza na maajabu ambayo Mungu alitenda kwa mikono yao kati ya watu wa mataifa mengine.

13. Walipomaliza kuongea, Yakobo alianza kusema: “Ndugu zangu, nisikilizeni!

14. Simoni ameeleza jinsi Mungu hapo awali alivyojishughulisha na watu wa mataifa mengine, akachagua baadhi yao wawe watu wake.

15. Jambo hili ni sawa kabisa na maneno ya manabii, kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:

16. ‘Baada ya mambo haya nitarudi,na kujenga tena kile kibanda cha Daudi kilichoanguka;nitayatengeneza magofu yake na kukijenga tena.

Kusoma sura kamili Matendo 15