Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 14:23-28 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, kisha, kwa kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.

24. Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.

25. Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.

26. Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.

27. Walipofika huko Antiokia walifanya mkutano wa kanisa la mahali hapo, wakawapa taarifa juu ya mambo Mungu aliyofanya pamoja nao, na jinsi alivyowafungulia watu wa mataifa mengine mlango wa kuingia katika imani.

28. Wakakaa pamoja na wale waumini kwa muda mrefu.

Kusoma sura kamili Matendo 14