Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 14:22-26 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Waliwaimarisha waumini wa miji hiyo na kuwatia moyo wabaki imara katika imani. Wakawaambia, “Ni lazima sisi sote kupitia katika taabu nyingi ili tuingie katika ufalme wa Mungu.”

23. Waliteua wazee katika kila kanisa kwa ajili ya waumini, kisha, kwa kusali na kufunga, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana ambaye walikuwa wanamwamini.

24. Baada ya kupitia katika nchi ya Pisidia, walifika Pamfulia.

25. Baada ya kuhubiri ule ujumbe huko Perga, walikwenda Atalia.

26. Kutoka huko walisafiri kwa meli wakarudi Antiokia ambako hapo awali walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi wa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameitimiza.

Kusoma sura kamili Matendo 14