Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 13:49-52 Biblia Habari Njema (BHN)

49. Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.

50. Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.

51. Basi, mitume wakayakunguta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.

52. Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.

Kusoma sura kamili Matendo 13