Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 13:37-41 Biblia Habari Njema (BHN)

37. Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.

38. Kwa hiyo, jueni, ndugu zangu, kwamba kwa njia ya mtu huyu ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu;

39. na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya sheria.

40. Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:

41. ‘Sikilizeni enyi wenye madharau,shangaeni mpotee!Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu,ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.’”

Kusoma sura kamili Matendo 13