37. Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
38. Kwa hiyo, jueni, ndugu zangu, kwamba kwa njia ya mtu huyu ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu;
39. na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya sheria.
40. Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
41. ‘Sikilizeni enyi wenye madharau,shangaeni mpotee!Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu,ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.’”