Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 7:33-37 Biblia Habari Njema (BHN)

33. Yesu akamtenga na umati wa watu, akamtia vidole masikioni, akatema mate na kumgusa ulimi.

34. Kisha akatazama juu mbinguni, akapiga kite, akamwambia, “Efatha,” maana yake “Funguka.”

35. Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukafunguliwa, akaanza kusema sawasawa.

36. Yesu akawaamuru wasimwambie mtu juu ya jambo hilo. Lakini kadiri alivyowakataza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari hiyo.

37. Watu walishangaa sana, wakasema, “Amefanya yote vyema: Amewajalia viziwi kusikia, na mabubu kusema!”

Kusoma sura kamili Marko 7