Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 6:48-56 Biblia Habari Njema (BHN)

48. Basi, akawaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kupiga makasia, maana upepo ulikuwa unawapinga. Karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji, akataka kuwapita.

49. Lakini walipomwona akitembea juu ya maji, walidhani ni mzimu, wakapiga yowe.

50. Maana wote walipomwona waliogopa sana. Mara Yesu akasema nao, “Tulieni, ni mimi. Msiogope!”

51. Kisha akapanda mashuani walimokuwa, na upepo ukatulia. Nao wakashangaa sana,

52. kwa sababu hawakuwa bado wameelewa maana ya ile mikate. Akili zao zilikuwa bado zimepumbazika.

53. Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti, wakatia nanga.

54. Walipotoka mashuani watu walimtambua Yesu mara.

55. Basi, kwa haraka wakazunguka katika nchi ile yote, wakaanza kuwachukua wagonjwa wamelala juu ya mikeka yao, wakawapeleka kila mahali waliposikia Yesu yupo.

56. Kila mahali Yesu alipokwenda, vijijini, mijini au mashambani, watu waliwaweka wagonjwa uwanjani, wakamsihi waguse walau pindo la vazi lake. Nao wote waliomgusa walipona.

Kusoma sura kamili Marko 6