Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 6:46-54 Biblia Habari Njema (BHN)

46. Baada ya kuwaaga watu alikwenda mlimani kusali.

47. Ilipokuwa jioni, mashua ilikuwa katikati ya ziwa, naye alikuwa peke yake katika nchi kavu.

48. Basi, akawaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kupiga makasia, maana upepo ulikuwa unawapinga. Karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji, akataka kuwapita.

49. Lakini walipomwona akitembea juu ya maji, walidhani ni mzimu, wakapiga yowe.

50. Maana wote walipomwona waliogopa sana. Mara Yesu akasema nao, “Tulieni, ni mimi. Msiogope!”

51. Kisha akapanda mashuani walimokuwa, na upepo ukatulia. Nao wakashangaa sana,

52. kwa sababu hawakuwa bado wameelewa maana ya ile mikate. Akili zao zilikuwa bado zimepumbazika.

53. Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti, wakatia nanga.

54. Walipotoka mashuani watu walimtambua Yesu mara.

Kusoma sura kamili Marko 6