Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 6:42-51 Biblia Habari Njema (BHN)

42. Watu wote wakala, wakashiba.

43. Wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakajaza vikapu kumi na viwili.

44. Nao waliokula hiyo mikate walikuwa wanaume 5,000.

45. Mara Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie kwenda Bethsaida, ngambo ya ziwa, wakati yeye anauaga umati wa watu.

46. Baada ya kuwaaga watu alikwenda mlimani kusali.

47. Ilipokuwa jioni, mashua ilikuwa katikati ya ziwa, naye alikuwa peke yake katika nchi kavu.

48. Basi, akawaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kupiga makasia, maana upepo ulikuwa unawapinga. Karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji, akataka kuwapita.

49. Lakini walipomwona akitembea juu ya maji, walidhani ni mzimu, wakapiga yowe.

50. Maana wote walipomwona waliogopa sana. Mara Yesu akasema nao, “Tulieni, ni mimi. Msiogope!”

51. Kisha akapanda mashuani walimokuwa, na upepo ukatulia. Nao wakashangaa sana,

Kusoma sura kamili Marko 6