Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 14:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Yangaliweza kuuzwa kwa fedha kiasi cha dinari 300, wakapewa maskini!” Wakamkemea huyo mama.

6. Lakini Yesu akawaambia, “Mwacheni; kwa nini mnamsumbua? Amenitendea jambo jema.

7. Maskini mnao daima pamoja nanyi; mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaopenda. Lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.

8. Yeye amefanya alivyoweza; ameupaka mwili wangu marashi kuutayarisha kwa mazishi.

9. Nawaambieni kweli, popote ulimwenguni Habari Njema itakapohubiriwa, kitendo hiki alichofanya kitatajwa kwa kumkumbuka yeye.”

Kusoma sura kamili Marko 14