Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 14:48-54 Biblia Habari Njema (BHN)

48. Yesu akawaambia, “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyanganyi?

49. Kila siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini sasa lazima Maandiko Matakatifu yatimie.”

50. Hapo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.

51. Kulikuwa na kijana mmoja aliyekuwa anamfuata Yesu akiwa amevaa shuka. Nao wakajaribu kumkamata.

52. Lakini yeye akaponyoka, akaiachilia ile shuka, akakimbia uchi.

53. Basi, wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu ambapo makuhani wakuu wote, wazee na waalimu wa sheria walikuwa wamekutanika.

54. Petro alimfuata Yesu kwa mbali, akaingia ndani ya ua wa kuhani mkuu, akaketi pamoja na walinzi akiota moto.

Kusoma sura kamili Marko 14