Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 14:46-51 Biblia Habari Njema (BHN)

46. Basi, hao watu wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.

47. Mmoja wa wale waliokuwa wamesimama hapo pamoja na Yesu, akachomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.

48. Yesu akawaambia, “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyanganyi?

49. Kila siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini sasa lazima Maandiko Matakatifu yatimie.”

50. Hapo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.

51. Kulikuwa na kijana mmoja aliyekuwa anamfuata Yesu akiwa amevaa shuka. Nao wakajaribu kumkamata.

Kusoma sura kamili Marko 14