33. Muwe waangalifu na kesheni, maana hamjui wakati huo utafika lini.
34. Itakuwa kama mtu anayeondoka nyumbani kwenda safari akiwaachia watumishi wake madaraka, kila mmoja na kazi yake; akamwambia na mlinzi wa mlango awe macho.
35. Kesheni, basi, kwa maana hamjui mwenye nyumba atarudi lini; huenda ikawa jioni, usiku wa manane, alfajiri au asubuhi.
36. Kesheni ili akija ghafla asije akawakuta mmelala.
37. Ninayowaambieni nyinyi, nawaambia wote: Kesheni!”