Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 13:32-37 Biblia Habari Njema (BHN)

32. “Lakini, juu ya siku au saa hiyo hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana; Baba peke yake ndiye ajuaye.

33. Muwe waangalifu na kesheni, maana hamjui wakati huo utafika lini.

34. Itakuwa kama mtu anayeondoka nyumbani kwenda safari akiwaachia watumishi wake madaraka, kila mmoja na kazi yake; akamwambia na mlinzi wa mlango awe macho.

35. Kesheni, basi, kwa maana hamjui mwenye nyumba atarudi lini; huenda ikawa jioni, usiku wa manane, alfajiri au asubuhi.

36. Kesheni ili akija ghafla asije akawakuta mmelala.

37. Ninayowaambieni nyinyi, nawaambia wote: Kesheni!”

Kusoma sura kamili Marko 13