Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 13:14-20 Biblia Habari Njema (BHN)

14. “Mtakapoona ‘Chukizo Haribifu limesimama mahali ambapo si pake, (msomaji na atambue maana yake), hapo, walioko Yudea wakimbilie milimani.

15. Aliye juu ya paa la nyumba asishuke kuingia nyumbani mwake kuchukua kitu.

16. Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.

17. Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!

18. Ombeni ili mambo hayo yasitukie nyakati za baridi.

19. Maana wakati huo kutakuwa na dhiki ambayo haijatokea tangu Mungu alipoumba ulimwengu mpaka leo, wala haitatokea tena.

20. Kama Bwana asingepunguza siku hizo hakuna binadamu ambaye angeokolewa. Lakini kwa ajili ya wateule wake, Bwana amezipunguza siku hizo.

Kusoma sura kamili Marko 13