Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 13:12-18 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe; baba atamsaliti mwanawe; watoto nao watawashambulia wazazi wao na kuwaua.

13. Watu wote watawachukieni nyinyi kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.

14. “Mtakapoona ‘Chukizo Haribifu limesimama mahali ambapo si pake, (msomaji na atambue maana yake), hapo, walioko Yudea wakimbilie milimani.

15. Aliye juu ya paa la nyumba asishuke kuingia nyumbani mwake kuchukua kitu.

16. Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.

17. Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!

18. Ombeni ili mambo hayo yasitukie nyakati za baridi.

Kusoma sura kamili Marko 13