Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 10:2-16 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Basi, Mafarisayo wakamwendea, na kwa kumjaribu wakamwuliza, “Je, ni halali mume kumpa mkewe talaka?”

3. Yesu akawajibu, “Mose aliwapa maagizo gani?”

4. Nao wakasema, “Mose aliagiza mume kumpatia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”

5. Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia amri hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.

6. Lakini tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu aliumba mwanamume na mwanamke.

7. Hivyo mwanamume atawaacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake,

8. nao wawili watakuwa mwili mmoja. Kwa hiyo, wao si wawili tena bali mwili mmoja.

9. Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe.”

10. Walipoingia tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake walimwuliza juu ya jambo hilo.

11. Naye akawaambia, “Anayemwacha mkewe na kuoa mwingine, anazini dhidi ya mkewe.

12. Na mwanamke anayemwacha mumewe na kuolewa na mwingine anazini.”

13. Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.

14. Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa.

15. Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia humo.”

16. Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.

Kusoma sura kamili Marko 10