39. Basi, akaenda kila mahali huko Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40. Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba: “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41. Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka! Takasika!”