Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 1:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

2. Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:“Mungu alisema, ‘Namtuma mjumbe wangu akutangulie,ambaye atakutayarishia njia yako.’

3. Sauti ya mtu anaita jangwani:‘Mtayarishieni Bwana njia yake,nyosheni barabara zake.’”

4. Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.

5. Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.

6. Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na ukanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.

Kusoma sura kamili Marko 1