1. Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2. Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:“Mungu alisema, ‘Namtuma mjumbe wangu akutangulie,ambaye atakutayarishia njia yako.’
3. Sauti ya mtu anaita jangwani:‘Mtayarishieni Bwana njia yake,nyosheni barabara zake.’”
4. Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.