Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 9:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yesu aliwaita wale kumi na wawili, akawapa uwezo wa kuponya pepo wote, na uwezo wa kuponya wagonjwa.

2. Halafu akawatuma waende kuhubiri ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.

3. Akawaambia, “Mnaposafiri msichukue chochote: Msichukue fimbo, wala mkoba, wala chakula, wala fedha, wala hata koti la ziada.

4. Nyumba yoyote mtakayoingia na kukaribishwa, kaeni humo mpaka mtakapoondoka katika kijiji hicho.

Kusoma sura kamili Luka 9