Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 8:49-54 Biblia Habari Njema (BHN)

49. Alipokuwa bado akiongea, Yairo akaletewa habari kutoka nyumbani: “Binti yako amekwisha kufa, ya nini kumsumbua Mwalimu zaidi?”

50. Yesu aliposikia hayo akamwambia Yairo, “Usiogope; amini tu, naye atapona.”

51. Alipofika nyumbani hakumruhusu mtu kuingia ndani pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohane, Yakobo na wazazi wa huyo msichana.

52. Watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili yake. Lakini Yesu akawaambia, “Msilie, kwa maana mtoto hajafa, amelala tu!”

53. Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.

54. Lakini Yesu akamshika mkono akasema, “Mtoto, amka!”

Kusoma sura kamili Luka 8