Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 8:20-23 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumwona.

21. Lakini Yesu akawaambia watu wote, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika.”

22. Siku moja, Yesu alipanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvuke ziwa twende mpaka ngambo.” Basi, wakaanza safari.

23. Walipokuwa wanasafiri kwa mashua, Yesu alishikwa na usingizi, akalala. Dhoruba kali ikaanza kuvuma, maji yakaanza kuingia ndani ya mashua, wakawa katika hatari.

Kusoma sura kamili Luka 8