Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 7:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Baada ya kusema yale aliyotaka watu wasikie, Yesu alikwenda Kafarnaumu.

2. Huko kulikuwa na jemadari mmoja ambaye alikuwa na mtumishi wake aliyempenda sana. Huyu mtumishi alikuwa mgonjwa karibu na kufa.

3. Yule jemadari aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee fulani Wayahudi waende kumwomba aje kumponya mtumishi wake.

4. Walipofika kwa Yesu, walimsihi sana, wakasema: “Huyu anastahili afanyiwe jambo hilo,

5. kwa maana yeye analipenda taifa letu, na ndiye aliyetujengea lile sunagogi.”

6. Basi, Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu na kufika nyumbani kwa yule jemadari, yule jemadari aliwatuma marafiki zake wamwambie Yesu: “Bwana, usijisumbue zaidi, maana mimi sistahili uingie nyumbani mwangu.

7. Ndio maana sikujiona nastahili hata kuja kwako. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona.

Kusoma sura kamili Luka 7