Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 7:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Baada ya kusema yale aliyotaka watu wasikie, Yesu alikwenda Kafarnaumu.

2. Huko kulikuwa na jemadari mmoja ambaye alikuwa na mtumishi wake aliyempenda sana. Huyu mtumishi alikuwa mgonjwa karibu na kufa.

3. Yule jemadari aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee fulani Wayahudi waende kumwomba aje kumponya mtumishi wake.

4. Walipofika kwa Yesu, walimsihi sana, wakasema: “Huyu anastahili afanyiwe jambo hilo,

5. kwa maana yeye analipenda taifa letu, na ndiye aliyetujengea lile sunagogi.”

Kusoma sura kamili Luka 7