Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 6:29-34 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie pia la pili. Mtu akikunyanganya koti lako mwachie pia shati lako.

30. Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyanganya mali yako usimtake akurudishie.

31. Jinsi mnavyotaka watu wawatendee nyinyi, watendeeni wao vivyo hivyo.

32. “Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda nyinyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.

33. Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya hayo.

34. Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile.

Kusoma sura kamili Luka 6