Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 6:25-31 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Ole wenu nyinyi mnaoshiba sasa,maana baadaye mtasikia njaa.Ole wenu nyinyi mnaocheka kwa furaha sasa,maana baadaye mtaomboleza na kulia.

26. Ole wenu nyinyi iwapo watu wote wanawasifu,maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.

27. “Lakini nawaambieni nyinyi mnaonisikiliza, wapendeni maadui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.

28. Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.

29. Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie pia la pili. Mtu akikunyanganya koti lako mwachie pia shati lako.

30. Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyanganya mali yako usimtake akurudishie.

31. Jinsi mnavyotaka watu wawatendee nyinyi, watendeeni wao vivyo hivyo.

Kusoma sura kamili Luka 6