Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 24:43-47 Biblia Habari Njema (BHN)

43. Akakichukua, akala, wote wakimwona.

44. Halafu akawaambia, “Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: Kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi.”

45. Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.

46. Akawaambia, “Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu,

47. na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia Yerusalemu, yahubiriwe kwamba watu wanapaswa kutubu na kusamehewa dhambi.

Kusoma sura kamili Luka 24