Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 24:39-53 Biblia Habari Njema (BHN)

39. Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkaone, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo.”

40. Baada ya kusema hayo, akawaonesha mikono na miguu.

41. Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, “Mnacho chakula chochote hapa?”

42. Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.

43. Akakichukua, akala, wote wakimwona.

44. Halafu akawaambia, “Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: Kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi.”

45. Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.

46. Akawaambia, “Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu,

47. na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia Yerusalemu, yahubiriwe kwamba watu wanapaswa kutubu na kusamehewa dhambi.

48. Nyinyi ni mashahidi wa mambo hayo.

49. Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu.”

50. Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.

51. Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.

52. Wao wakamwabudu, kisha wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:

53. Wakakaa muda wote hekaluni wakimsifu Mungu.

Kusoma sura kamili Luka 24