18. Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!” (
19. Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20. Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21. lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
22. Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya ubaya gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”