Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 23:18-22 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!” (

19. Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)

20. Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;

21. lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”

22. Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya ubaya gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”

Kusoma sura kamili Luka 23