Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 22:62-71 Biblia Habari Njema (BHN)

62. Hapo akatoka nje, akalia sana.

63. Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.

64. Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri, tuone!”

65. Wakamtolea maneno mengi ya matusi.

66. Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na waalimu wa sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.

67. Nao wakamwambia, “Tuambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;

68. na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.

69. Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenye Nguvu.”

70. Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Nyinyi mnasema kwamba mimi ndiye.”

71. Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”

Kusoma sura kamili Luka 22