Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 22:57-63 Biblia Habari Njema (BHN)

57. Lakini Petro akakana akisema, “Wee! Simjui mimi.”

58. Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana wee; si mimi!”

59. Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”

60. Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.

61. Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”

62. Hapo akatoka nje, akalia sana.

63. Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.

Kusoma sura kamili Luka 22