Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 22:14-19 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.

15. Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.

16. Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika ufalme wa Mungu.”

17. Kisha akatwaa kikombe cha divai, akashukuru, akasema, “Pokeeni, mgawane.

18. Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka ufalme wa Mungu utakapokuja.”

19. Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”

Kusoma sura kamili Luka 22