Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 20:21-26 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.

22. Basi, tuambie kama ni halali au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”

23. Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,

24. “Nionesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”

25. Nao wakamjibu, “Ni ya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, ya Kaisari mpeni Kaisari, na ya Mungu mpeni Mungu.”

26. Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.

Kusoma sura kamili Luka 20