Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 2:47-52 Biblia Habari Njema (BHN)

47. Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.

48. Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutendea hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”

49. Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”

50. Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.

51. Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.

52. Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.

Kusoma sura kamili Luka 2