Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 2:26-31 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.

27. Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na sheria,

28. Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu, akisema:

29. “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako,umruhusu mtumishi wako aende kwa amani.

30. Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu ulioleta,

31. ambao umeutayarisha uonekane na watu wote:

Kusoma sura kamili Luka 2