26. Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27. Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na sheria,
28. Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu, akisema:
29. “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako,umruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30. Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu ulioleta,
31. ambao umeutayarisha uonekane na watu wote: