Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 2:23-34 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Katika sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”

24. Pia walikwenda ili watoe sadaka: Hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika sheria ya Bwana.

25. Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.

26. Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.

27. Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na sheria,

28. Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu, akisema:

29. “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako,umruhusu mtumishi wako aende kwa amani.

30. Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu ulioleta,

31. ambao umeutayarisha uonekane na watu wote:

32. Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa,na utukufu kwa watu wako Israeli.”

33. Baba yake Yesu na mama yake walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.

34. Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;

Kusoma sura kamili Luka 2