Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 2:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote nchini kote wahesabiwe.

2. Sensa hiyo ilikuwa mara ya kwanza, wakati Kurenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.

3. Basi, wote waliohusika walikwenda kuhesabiwa kila mtu katika mji wake.

4. Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya, na kwa vile alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi, alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yudea, alikozaliwa mfalme Daudi.

5. Alikwenda kuhesabiwa pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mjamzito.

Kusoma sura kamili Luka 2