Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 19:43-48 Biblia Habari Njema (BHN)

43. Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.

44. Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”

45. Kisha, Yesu aliingia hekaluni, akaanza kuwafukuza nje wafanyabiashara

46. akisema, “Imeandikwa: ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala’; lakini nyinyi mmeifanya kuwa pango la wanyanganyi.”

47. Yesu akawa anafundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu, waalimu wa sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,

48. lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

Kusoma sura kamili Luka 19