Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 18:33-42 Biblia Habari Njema (BHN)

33. Watampiga mijeledi na kumuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”

34. Lakini wao hawakuelewa jambo hilo hata kidogo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.

35. Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.

36. Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”

37. Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”

38. Naye akapaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”

39. Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: “Mwana wa Daudi, nihurumie!”

40. Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,

41. “Unataka nikufanyie nini?” Naye akamjibu, “Bwana, naomba nipate kuona.”

42. Yesu akamwambia, “Ona! Imani yako imekuponya.”

Kusoma sura kamili Luka 18