Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 17:9-17 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Je, utamshukuru huyo mtumishi kwa sababu ametimiza aliyoamriwa?

10. Hali kadhalika na nyinyi mkisha fanya yote mliyoamriwa, semeni: ‘Sisi ni watumishi tusio na faida, tumetimiza tu yale tuliyotakiwa kufanya.’”

11. Yesu akiwa safarini kwenda Yerusalemu alipitia katika mipaka ya Samaria na Galilaya.

12. Alipokuwa anaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wenye ukoma walikutana naye, wakasimama kwa mbali.

13. Wakapaza sauti wakisema, “Yesu Mwalimu, tuonee huruma!”

14. Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajioneshe kwa makuhani.” Basi, ikawa walipokuwa wanakwenda, wakatakasika.

15. Mmoja wao alipoona kwamba ameponywa, alirudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa.

16. Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru. Huyo alikuwa Msamaria.

17. Hapo Yesu akasema, “Je, si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi?

Kusoma sura kamili Luka 17