Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 17:31-37 Biblia Habari Njema (BHN)

31. “Siku hiyo, yeyote atakayekuwa juu ya paa asishuke kwenda nyumbani kuchukua mali yake. Kadhalika, naye atakayekuwa shambani asirudi nyuma.

32. Kumbukeni yaliyompata mke wa Loti.

33. Yeyote anayetaka kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na yeyote anayeipoteza, ataiokoa.

34. Nawaambieni, siku ile usiku watu wawili watakuwa wanalala pamoja, mmoja atachukuliwa na yule mwingine ataachwa.

35. Wanawake wawili watakuwa wakisaga nafaka pamoja; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.” [

36. Watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]

37. Hapo wakamwuliza, “Ni wapi Bwana?” Naye akawaambia, “Palipo mzoga, ndipo tai watakapokusanyikia.”

Kusoma sura kamili Luka 17