Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 17:12-20 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Alipokuwa anaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wenye ukoma walikutana naye, wakasimama kwa mbali.

13. Wakapaza sauti wakisema, “Yesu Mwalimu, tuonee huruma!”

14. Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajioneshe kwa makuhani.” Basi, ikawa walipokuwa wanakwenda, wakatakasika.

15. Mmoja wao alipoona kwamba ameponywa, alirudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa.

16. Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru. Huyo alikuwa Msamaria.

17. Hapo Yesu akasema, “Je, si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi?

18. Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu ila tu huyu mgeni?”

19. Halafu akamwambia huyo mtu, “Simama, uende zako; imani yako imekuponya.”

20. Wakati mmoja, Mafarisayo walimwuliza Yesu, “Ufalme wa Mungu utakuja lini?” Naye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa namna itakayoweza kuonekana.

Kusoma sura kamili Luka 17