Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 17:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha.

2. Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa.

3. Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe.

4. Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema, ‘Nimetubu,’ lazima umsamehe.”

5. Mitume wakamwambia Bwana, “Utuongezee imani.”

Kusoma sura kamili Luka 17