Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 15:3-6 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Yesu akawajibu kwa mfano:

4. “Hivi, mmoja wenu akiwa na kondoo 100, akigundua kwamba mmoja wao amepotea, atafanya nini? Atawaacha wale tisini na tisa mbugani, na kwenda kumtafuta yule aliyepotea mpaka ampate.

5. Akimpata, atambeba mabegani kwa furaha.

6. Anapofika nyumbani, atawaita rafiki zake na kuwaambia, ‘Furahini pamoja nami, kwa sababu nimempata yule kondoo wangu aliyepotea.’

Kusoma sura kamili Luka 15