Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 15:13-17 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Baada ya siku chache, yule mdogo aliuza urithi wake, akasafiri na fedha aliyopata, akaenda nchi ya mbali ambako aliitumia ovyo.

14. Alipomaliza kutumia kila kitu, kukatokea njaa kali katika nchi ile, naye akaanza kuhangaika.

15. Akaomba kazi kwa mwananchi mmoja wa huko naye akampeleka shambani mwake kulisha nguruwe.

16. Alitamani kula maganda waliyokula wale nguruwe, ila hakuna mtu aliyempa kitu.

17. Alipoanza kupata akili, akafikiri: ‘Mbona kuna wafanyakazi wengi wa baba yangu wanaokula na kusaza, nami ninakufa njaa?

Kusoma sura kamili Luka 15