Agano la Kale

Agano Jipya

Luka 12:28-35 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Ikiwa basi, Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, si atawafanyia nyinyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!

29. “Basi, msivurugike akili, mkihangaika juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.

30. Kwa maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wote wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.

31. Shughulikeni kwanza juu ya ufalme wa Mungu, na hayo mtapewa kwa ziada.

32. “Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni ufalme.

33. Uzeni mali yenu mkawape maskini hizo fedha. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na kujiwekea hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.

34. Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.

35. “Muwe tayari mmejifunga mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;

Kusoma sura kamili Luka 12